Na mwanafunzi wetu: James Mwakyembe
Polisi mkoani Mbeya
wanamshikiria Brown Mensah (25) mkazi wa Songea kwa kumiliki bunduki aina ya
gobole na risasi saba za shot gun.
Mtuhumiwa huyo alikamatwa mnamo tarehe 12-04-2014 majira ya
saa kumi na moja na nusu jioni katika mtaa wa Mwaka-Tunduma kata na tarafa ya
Tunduma, wilaya ya Momba mkoa wa Mbeya.
Aidha mtuhumiwa huyo baada ya kufikishwa kituo cha polisi
Tunduma na kufanyika upekuzi alikutwa na noti bandia,moja ya Tshs 10,000/= yenye namba BX-5273247, zingine kumi
na saba za Tshs 5,000/= zenye namba AA-08459261 na noti zingine ishirini na
tatu za Tshs 2,000/= zenye namba CK-1942911. Taratibu za kumfikisha mtuhumiwa
mahakamani zinaendelea.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya, kamishina mwandamizi wajeshi la
polisi Ahmed Z. Msangi ametoa wito kwa jamii kufuata taratibu za kumiliki
silaha.
0 comments:
Post a Comment