Our Collegues

Courses offered:- Certificate in Digital Journalism (CDJ), Certificate in Radio Production (CRP), our main campus are based at Nane nane Mbeya!

Usajiri wa Wanafunzi wapya Umeanza

Muhula wa masomo unaanza tarehe 10, April 2014 kwa kozi za Digital Journalism na Radio Production ngazi ya cheti kwa mwaka mmoja tu. Kwa maelezo zaidi tupigie simu 0763 099842 au 0654634163 karibuni sana!

Our Collegues

Courses offered:- Certificate in Digital Journalism (CDJ), Certificate in Radio Production (CRP), our main campus are based at Nane nane Mbeya!

Usajiri wa Wanafunzi wapya Umeanza

Muhula wa masomo unaanza tarehe 10, April 2014 kwa kozi za Digital Journalism na Radio Production ngazi ya cheti kwa mwaka mmoja tu. Kwa maelezo zaidi tupigie simu 0763 099842 au 0654634163 karibuni sana!

Tuna miundo mbinu mizuri kwa ajiri ya mafunzo

Mafunzo ya vitendo/field kwa wanafunzi wa DMCT..

Thursday, April 24, 2014

Waziri Mkuu Malaysia akataa kuthibitisha kama abiria waliokuwa kwenye ndege iliyopotea walifariki.


 


Ni zaidi ya wiki sita sasa baada ya ndege ya Malaysia FH370 kutoweka, waziri mkuu Malaysia amesema serikali yake bado haiko tayari kutangaza kuwa watu 239 waliokuwemo kwenye ndege hiyo wamepoteza maisha.
"Kwasasa siko tayari kuzungumzia suala hili nadhani jambo muhimu ni kuheshimu hisia za watu waliopoteza ndugu zao na ukizingatia walishawahi kusema hawatakubaliana na hili mpaka watakapoona ushahidi alisema waziri, Najib Razak.
Hata hivyo, alisema , ni " vigumu kufikiria vinginevyo."
Najib pia aliongeza kuwa serikali yake itatoa reporti ya awali wiki ijayo juu ya kupotea kwa ndege hiyo ambapo tayari ripoti hiyo imeshafikishwa katika Umoja wa Mataifa.
'Mwezi mmoja uliopita, Najib alitangaza kuwa , kwa kuzingatia data zilizopatikana katika satellite ya Inmarsat , wachunguzi walibainisha kuwa kwa mara ya mwisho ndege hiyo ilidondoka katikati ya Bahari ya Hindi, magharibi eneo la Perth na kwamba eneo hilo lipo kijijini na kwa ushahidi huo alisikitika kuwaambia ndugu wa waliopotea kwamba ndege hiyo ilianguka kusini mwa Bahari ya Hindi. '

Friday, April 18, 2014

Polisi mkoani Mbeya wanamshikiria Brown Mensah (25) mkazi wa Songea kwa kumiliki bunduki aina ya gobole na risasi saba za shot gun.



Na mwanafunzi wetu: James Mwakyembe



Polisi  mkoani Mbeya wanamshikiria Brown Mensah (25) mkazi wa Songea kwa kumiliki bunduki aina ya gobole na risasi saba za shot gun.
Mtuhumiwa huyo alikamatwa mnamo tarehe 12-04-2014 majira ya saa kumi na moja na nusu jioni katika mtaa wa Mwaka-Tunduma kata na tarafa ya Tunduma, wilaya ya Momba mkoa wa Mbeya.

Aidha mtuhumiwa huyo baada ya kufikishwa kituo cha polisi Tunduma na kufanyika upekuzi alikutwa na noti bandia,moja ya  Tshs 10,000/= yenye namba BX-5273247, zingine kumi na saba za Tshs 5,000/= zenye namba AA-08459261 na noti zingine ishirini na tatu za Tshs 2,000/= zenye namba CK-1942911. Taratibu za kumfikisha mtuhumiwa mahakamani zinaendelea.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya, kamishina mwandamizi wajeshi la  polisi Ahmed Z. Msangi ametoa wito kwa jamii kufuata taratibu za kumiliki silaha.

Mtu mmoja aliyetambuliwa kwa jna la Joshua Paul (31) mkazi wa kijiji cha Ntokela wilayan Rungwe ameuawa na watu wasiofahamika na kutupwa kwenye shamba la mahindi.



Na mwanafunzi wetu James Mwakyembe



Mtu mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Joshua Paul (31) mkazi wa kijiji cha Ntokela wilayani Rungwe ameuawa na watu wasiofahamika na kutupwa kwenye shamba la mahindi jana jioni.

Akifafanua zaidi kuhusu tukio hilo kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya, kamishina mwandamizi wa jeshi la polisi Ahmed Z. Msangi amesema, mwili wa marehemu ulikutwa kwenye shamba la mahindi linalomilikiwa na bwana Yohana Mbilinyi, ukiwa umekatwa kitu chenye ncha kali sehemu ya paji la uso na kifuani. 

Bwana Msangi ameongeza kuwa tayari polisi wanamshikiria Belisi Sikakinda (28) mkazi wa kijiji cha Kiwira wilayani Rungwe, ambaye alikuwa na marehemu siku ya mwisho, huku uchunguzi zaidi kuhusu tukio hilo ukiendelea kufanyika.

Kamanda Msangi ametoa wito kwa jamii kushirikiana na jeshi la polisi ili kuwabaini wahusika wa mauaji hayo na sheria ichukue mkondo dhidi yao.

Friday, April 4, 2014

World Radio Day at Vatican Radio



As the Grandmother of radio stations (she turned 83 on
February 12th), Vatican Radio was proud to inaugurate
World Radio Day 2014 (one second after midnight on
February 13th) by broadcasting a concert performed by
the French National Orchestra and offered by Radio
France and the European Broadcasting Union (EBU).
Special programming, available throughout the day on
website (www.vatican radio.org), focused on the role of
women in broadcasting and how Vatican Radio’s own
female journalists are able to give voice to women
without a voice. Part of a long-term project involving
women from Africa, Asia and the Americas, these
programmes highlighted courageous and inspiring
women who face challenging situations as they work for
peace and justice in the world.
Listen the programmes here: Vatican Radio
programmes on WRD 2014 by UNESCO World Radio Day