Our Collegues

Courses offered:- Certificate in Digital Journalism (CDJ), Certificate in Radio Production (CRP), our main campus are based at Nane nane Mbeya!

Usajiri wa Wanafunzi wapya Umeanza

Muhula wa masomo unaanza tarehe 10, April 2014 kwa kozi za Digital Journalism na Radio Production ngazi ya cheti kwa mwaka mmoja tu. Kwa maelezo zaidi tupigie simu 0763 099842 au 0654634163 karibuni sana!

Our Collegues

Courses offered:- Certificate in Digital Journalism (CDJ), Certificate in Radio Production (CRP), our main campus are based at Nane nane Mbeya!

Usajiri wa Wanafunzi wapya Umeanza

Muhula wa masomo unaanza tarehe 10, April 2014 kwa kozi za Digital Journalism na Radio Production ngazi ya cheti kwa mwaka mmoja tu. Kwa maelezo zaidi tupigie simu 0763 099842 au 0654634163 karibuni sana!

Tuna miundo mbinu mizuri kwa ajiri ya mafunzo

Mafunzo ya vitendo/field kwa wanafunzi wa DMCT..

Thursday, January 16, 2014

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, amesema kuwa jeshi la Uganda linashirikiana na wanajeshi wa Sudan kusini kupambana na waasi wa Sudan Kusini.


Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, amesema kuwa jeshi la Uganda linashirikiana na wanajeshi wa Sudan kusini kupambana na waasi wa Sudan Kusini.

Mapigano hayo ambayo yalizuka mwezi uliopita yanaendelea katika maeneo kadhaa ya Sudan kusini, licha ya kufufuliwa kwa mazungumzo ya amani katika nchi jirani ya Ethiopia .
Baada ya wiki kadhaa za tetesi za wanjeshi wa Uganda kuwa nchini Sudan Kusini, jeshi la Uganda sasa limekiri rasmi kuwa liko katika vita na waasi wa Sudan Kusini.
Kwa mujibu wa msemaji wa jeshi, Luteni Kanali Paddy Ankunda, Uganda ina takriban wanajeshi elfu moja na mia sita nchini humo.

Serikali ya Uganda imekiri kukabiliana na waasi hao tangu mwanzoni mwa wiki hii,wakati wanajeshi hao waliposhambuliwa na waasi wanaoongozwa na makamu wa zamani wa Rais Riek Machar.

Akisimulia kuhusu tukio hilo kwenye mkutano wa kikanda nchini Angola mnamo Jumatano, Rais Yoweri Museveni, alisema kwamba baadhi ya wanajeshi wake waliuawa au kujeruhiwa.
Jeshi la Uganda hata hivyo halijaeleza idadi kamili ya wanajeshi waliouawa.
Luteni Kanali Paddy Ankunda ametetea hatua ya Uganda kupeleka wanajeshi wake Sudan Kusini ikisema lengo lake ni kulinda raia na kufungua njia kwa misaada kuingizwa nchini humo .
Serikali ya Uganda imekuwa ikiunga mkono kikamilifu serikali ya Rais Salva Kiir ikisema kwamba imechaguliwa kidemokrasia wakati Riek Machar anataka kunyakua madaraka kwa nguvu.
Uganda ina maslahi nchini Sudan Kusini. Ni kituo rasmi cha kuuza bidhaa zake na kituo ambacho waasi wa Joseph Kony wamekuwa wakipigania na kutatiza serikali ya Museveni ingawa sasa wamedhibitwa.

Chanzo: BBC Swahili

Sunday, January 12, 2014

Chuo cha Digital Media College of Tanzania-DMCT kufunguliwa jumatano tarehe 15/01/2014


Chuo cha Digital Media College of Tanzania-DMCT kufunguliwa jumatano tarehe 15/01/2014. chuo hiki ambacho kitaanza kutoa kozi mbili kwa ngazi ya cheti kinatarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika tanisia ya habari! Katika kuhakikisha utekelezaji wa mabadiliko hayo chuo hiki kitafundisha kozi ya Digital(Online) Journalism pamoja na Radio Production kwa ngazi ya cheti.

Kutokana na wingi wa vyuo vya uandishi wa habari ni dhahiri kwamba wanafunzi wengi wamekuwa wakimaliza masomo na kurudi nyumbani bila mafanikio yoyote ya kupata ajira. Ni jambo la kusikitisha kwa sababu wametumia gharama kupata elimu hiyo ili iwasaidie, lakini pia inasikitisha kukosa kazi wakati habari ni chakula cha kila siku ambacho binadamu anakihitaji bila kushiba! Hakuna mtu anayetosheka na habari, bali kila siku watu wanahitaji habari hivyo mhitimu wa fani ya uandishi wa habari kukosa kazi ni moja ya madhaifu yaliyopo katika vyuo vya uandishi wa habari.

Akielezea Mkurugenzi wa DMCT Bw. Lucas Kulwa alisema kuwa, DMCT imejipanga kuhakikisha kuwa matunda makubwa yanaanza kupatikana mapema kupitia chuo hiki kwa kutoa wanafunzi wenye kiwango cha juu. Aidha katika kuhakikisha hilo, wanafunzi wa DMCT wataanza na kozi ya kiingereza kwa level ya kati ndani ya mwezi mmoja! Akiliendelea kusimulia Bw. Lucas alisema, huwezi kuwa mwandishi wa habari mzuri kama hata kiingereza hujui, dunia ya leo inawasiliana kwa lugha hii ambayo tunaweza kusema ndiyo lugha inayotumiwa na watu wengi duniani.

Hivyo ili uwe mwandishi wa habari mzuri ni lazima ukubali kujifunza na kuongea kiingereza kwa ufasaha! Pia DMCT itatoa kozi ya computer kwa muda wa mwezi mmoja mara tu baada ya kozi ya kiingereza kumalizika. Pia kwakuwa tumenuia kufundisha uandishi wa habari wa kidigitali hatuna budi kuhakikisha wanafunzi wote wanaongea kiingereza na kutumia computer kwa ufasaha!

DMCT itawawezesha wanafunzi wake kuanza kujipatia kipato cha pesa kutokana na kazi za vitendo watakazokuwa wakifanya kama kuandika habari, pamoja na mafunzo ya kumiliki mitandao yatakapofundishwa! Tunatarajia kila mwanafunzi aweze kumiliki blog yake ambayo ataiwekea habari nzuri na zenye tija kila wakati.

Chuo pia kina mikakati mbalimbali kama Tour za nje ya nchi kwenda kujifunza wenzetu wanafanye zaidi. Mtandao huu unakuahidi kuwa utaendelea kukupasha habari mbalimbali kuhusu chuo hiki usikose kuendelea kufuatilia mtandao wetu.